Wednesday, May 22, 2013

BREAKING NEWS: GESI YA MTWARA KIMENUKA

 Habari zilizotufikia kutoka Mtwara zinaeleza kuwa kumeibuka vurugu ambazo zimepelekea mabomu ya machozi na risasi za moto kutumika baada ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kusomwa bungeni na kueleza kuwa mradi wa gesi Mtwara utatekelezwa bila kutaja faida za moja kwa moja watakazozipata wananchi hao. Inadaiwa kuwa kwa sasa kauli mbiu ya wananchi walio katika maeneo hayo ni  "Gesi haitoki hata kwa bomba la peni". Inaelezwa kuwa kituo cha mafuta cha Total kimechomwa moto wakati wa vurugu hizo. Katika kukabiliana na vurugu hizo, inadaiwa polisi kutoka Masasi na Lindi wapo eneo hilo kuongeza nguvu. Taarifa zaidi zitawajia hivi punde

No comments: