Wednesday, July 4, 2012

Banda la Wizara ya Fedha, lachukua ushindi wa pili kwenye Maonesho ya Sabasaba

Mchumi Mwandamizi wa Wizara ya Fedha, Idara ya Bajeti, Adam Msumule, akimpatia maelezo mwananchi aliyetembelea banda la wizara ya Fedha, kuhusu bejeti ya nchi, kwenye maonesho ya Biashara ya Kimataifa, viwanja vya J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Fedha wanaotoa huduma ya kuwaelimisha wananchi kwenye banda la wizara hiyo, Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, wakipiga picha ya pamoja kwa ajili ya kumbukumbu ya maonesho hayo leo




Wananchi wakiingia kwenye banda la Wizara ya Fedha, leo kujionea na kupata huduma mbalimbali zitolewazo na wizara hiyo.

No comments: