Thursday, July 5, 2012

TWIGA BANCORP WATOA HUDUMA KAMILI ZA KIBENKI KATIKA MAONYESHO YA KIMATAIFA YA SABASABA

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Twiga Bancorp ambao wapo kwa ajili ya kutoa huduma katika banda la Benki hiyo katika viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara maarufu Saba Saba wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya Banda lao linalotoa huduma kamili za Kibenki.





Afisa Masoko wa Twiga Bancorp Limited, Adelbert Archerd Tibikunda akiwa amekamatia tuzo ya Century International Gold Quality ERA waliyo ipata Genever kwa huduma bora .




Katika Banda la Twiga Bancorp wateja wanapata fursa ya kuweka fedha zao papo hapo baada ya kufanya mauzo ndani ya Saba Saba. Yanini utembee na fedha nyingi wakati Benki ya twiga ipo nawe pale ulipo.



Fedha katika ATM ni kwa saa 24, siku 7 za  wiki, mwezi mzima na siku 360. Huduma hii katika banda la Twiga hafungwi mwaka mzima.



Utoa huduma bora ndio nguzo na ngao ya Twiga Bancorp, pichani ni mteja akiwa na furaha wakati akizungumza na Afisa Mwandamizi  Mwendeshaji wa Benki ya Twiga Bancorp Limited, Lydia Matembel, alipotembelea banda lao katika viwanja vya Maonesho Saba Saba.
Ofisa wa Benki ya Twiga Bancorp Limited, Ernest Kikwasi, akitoa maelezo kwa wananchi  waliotembelea banda hilo jana juu ya akaunti maalum ya watoto. Twiga Bancorp ni miongoni mwa benki zinazoshiriki katika Maonesho ya 36 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu JK Nyerere barabara ya Kilwa huku wakitoa huduma kamili za kibenki.
 Mmteja wa Twiga Bancorp akitoka kupata huduma katika banda la Benki hiyo kwa furaha baada ya kufanikiwa kutimiza alichotaka kwa wakati.




No comments: