Thursday, July 5, 2012

SABABU ZA YANGA KUTOLEWA KWENYE MASHINDANO YA URAFIKI.

CHAMA cha Soka Zanzibar (ZFA) kimewafukuza Yanga katika mashindano ya Urafiki kwa kitendo cha kupeleka kikosi cha vijana (Yanga B) badala ya kikosi cha wakubwa kwenye michuano hiyo kama walivyokubaliana.
ZFA na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa ujumla wamekerwa na kitendo kilichofanywa na uongozi wa Yanga na wamekichukulia kama ni dharau, kupeleka timu B badala ya timu A. (Stori imeandikwa na Bin Zubery)

No comments: