Friday, August 10, 2012

Hali ya uuzaji wa madawa ya binadamu kiholela jijini Dar Es Salaam inatisha

Matokeo haya yametokana na utafuti ulifanywa na YITA Novemba 2011 na ulihusisha watafitit waliofanya ziara siri (mystery shoppers) 126 katika maduka 64 ya wilaya zote tatu za Dar es salaam. Jina la muhtasari wenye matokeo hayo ni “Ununuzi wa dawa jijini Dar es Salaam-Je, maduka ya dawa yanazingatia kanuni?” . Pamoja na mengine watafiti waliweza kuhoji yafuatayo;

    Je, dawa zinaweza kutufanya wagonjwa? Je, zinatolewa ipasavyo? Na je, mfumo wa kuwalinda wananchi kutokana na madhara ya matumizi mabaya ya dawa unafanya kazi vizuri?

    Ikumbukwe mamlaka ya dawa na chakula Tanzania imetamka wazi kwenye  Kifungu cha 31:3 ya viwango vya biashara ya dawa nchini ya mwaka 2006 (Pharmaceutical Business Standards Regulations) kuwa;

    “Hakuna mtoaji dawa yeyote atakayetoa dawa ambazo matumizi yake yanapaswa kuwa kwa maagizo ya daktari tu isipokuwa kwa agizo la matumizi ya dawa husika lililotolewa na mfanyakazi wa afya, mganga wa meno au wa mifugo au mtu mwingine yeyote aliyeidhinishwa kuagiza matumizi ya dawa”.

    Utaafiti imedhihirisha ukiukwaji mkubwa wa kanuni za Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).Ni wazi madhara yafuatayo yataliandama Taifa kama hatua za dhati hazitachukuliwa haraka;

No comments: