Tuesday, August 7, 2012

MADHARA YA UNENE, YANASHINDA YA UVUTAJI SIGARA!

TAARIFA hii inaweza kuwashangaza baadhi ya watu, lakini takwimu zilizotolewa hivi karibuni zilizowahusisha zaidi ya watu 60,000 nchini Kanada, zinaonesha kwamba unene una madhara zaidi kuliko uvutaji sigara.

Taarifa kwamba unene ni hatari kwa afya, unaweza kuwashangaza watu wengi hasa ukizingatia kwamba hivi sasa watu kuwa wanene na wenye matumbo makubwa, limekuwa ni jambo la kifahari na la kawaida.

Utafiti huo unaonesha pia kuwa kama kusingekuwepo na tatizo la unene wa kupindukia (obesity) kwa watu wengi duniani, basi safari za kwenda hospitali kwa matatizo mbalimbali ya kiafya, nayo yangepungua kwa zaidi ya asilimia 10.

UNENE WA KUPINDUKIA, CHANZO CHA MARADHI
Ni muhimu watu kuondokana na imani potofu kuwa unene ni dalili ya afya njema, badala yake waelewe kwamba unene wa kupindukia ni chanzo cha maradhi ukiwemo ugonjwa wa kisukari (diabetes type 2).

Licha ya vyakula vya mafuta mengi kuchangia unene, vyakula vingine vya kawaida vinavyoliwa na watu wengi, vimetajwa kuwa hatari zaidi kwa kuongeza unene.
Baadhi ya vyakula hivyo ni pamoja na keki, chips, vitumbua, maandazi, soda, nyama za kukaanga, unywaji wa soda, vinywaji vya kutia mwili nguvu (energy drinks) na vyakula vingine vitamu vitamu na vyenye sukari nyingi.

Ni ukweli ulio dhahiri kwamba, unene wa kupindukia una uhusiano mkubwa na magonjwa sugu na una athari pia katika umri wa kuishi binadamu na kwamba soda inachangia sana kuongeza uzito mwilini.

Kujua namna ya kuishi kwa kula vyakula kwa kuchagua kwa kigezo cha kula chenye faida tu mwilini, ndiyo dawa pekee na ya uhakika ya kujikinga na kupambana na maradhi hatari.

Pendelea kula vyakula asilia na jiepushe kula vyakula vilivyotayarishwa na kuhifadhiwa (vyakula vya makopo na vya kwenye maboksi) na badala yake pendelea kula vyakula asilia na vilivyo ‘fresh’. Kama ni nafaka, kula vyakul

Jiepushe na ulaji wa kiasi kingi cha sukari (kwa kupitia njia mbalimbali, kama soda, juisi, n.k), kwani sukari inachangia kwa kiasi kikubwa kudhoofisha kinga ya mwili na kuchochea chembechembe za saratani mwilini.

Hakikisha pia unafanya mazoezi mara kwa mara. Hata kama unakula chakula bora kuliko watu wote duniani, kama hufanyi mazoezi lazima utapatwa na matatizo ya kiafya. Mazoezi na shuruba za mara kwa mara, huongeza uzalishaji wa homoni za ukuaji wa mwili (Human growth hormone).

Hakikisha unakunywa maji safi na salama kwa wingi kila siku ili kuuweka utumbo wako safi. Kama inavyoelezwa, kifo huanzia tumboni, huna budi kuhakikisha tumbo lako linakuwa safi kila siku kwa kunywa maji ya kutosha yatayokuwezesha kupata choo kila siku na kwa kufanya hivyo utauweka utumbo wako safi.

Mwisho, hakikisha unapata muda wa kupumzika na kulala usingizi wa kutosha kila siku, kwani ukosefu wa usingizi na kuacha kupumzika vina athari sana kwenye uzalishaji wa homoni muhimu mwilini.

No comments: