Thursday, December 6, 2012

DAKTARI WA ‘MOI’ MUHIMBILI, NESI WAKE MBARONI KWA RUSHWA

 Daktari Matiko (katikati) akiongozwa na Afisa wa Takukuru (nyuma yake).  Aliyetangulia ni wakili anayemtetea, Paschal Kamala.
                                                                 …Akielekea kizimbani kwa upole.
                      Nesi KImwomwe (kulia) naye akielekea kizimbani kusomewa mashitaka yake.
                                           Uchungu wa safari ya kuelekea kizimbani.
                    Ndugu na jamaa wakifuata nyuma kwa ajili ya kusikiliza kesi za wapendwa wao.

DAKTARI wa hospitali ya Muhimbili Kitengo cha Mifupa (MOI), Deodata Kisasi Matiko (30) na nesi wake, Erick Petro Kimwomwe (28), leo wamepandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam wakishitakiwa kwa kuomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni moja waliyomwomba Stanford Aaron Mhina ili wamfanyie upasuaji wa mgongo ndugu yake aitwae Fanuel Daniel Gideon aliyelazwa Wodi ya Sewa Haji namba (18) Kitengo cha Mifupa (MOI). Imedaiwa kuwa mgonjwa huyo alipelekwa MOI baada ya kupewa rufaa na Hospitali ya Tumbi iliyopo Kibaha mkoani Pwani ambapo alifikishwa hospitalini hapo baada ya kupata ajali ya gari maeneo ya Kibaha na kuvunjika mgongo.
                                              

PICHA : RICHARD BUKOS / GPL  

No comments: