Saturday, January 5, 2013

Leo ikiwa ni siku ya kuwakumbuka Denis na Ismail chadema yafanya shughuli za kijamii...

 Moja ya vituo vya kulelea watoto yatima alivyo vitembelea Godbless Lema na katibu mkoa Amani
 Mh. Lema akiwa na watoto yatima kati ya vituo alivyotembelea leo katika siku ya kuwakumbuka Denis na Ismil.
 Huyu mtoto YATIMA ameshika nafasi ya tatu ktk Wilaya Arusha matokeo ya la saba..
CHADEMA Arusha leo itakuwa na Kumbukumbu ya miaka miwili (2) ya mauaji ya makusudi ya raia wasio kuwa na hatia yaliyotokea 5/1/2011.Kumbukumbu hii itaenda sambamba na chama kufanya shughuli za kijamii,ikiwepo kutembelea vituo vitano vya watoto yatima jijini Arusha,kutoa wafungwa waliofungwa kwa kukosa faini ya ela ndogo,kisha kuhitimishwa kwa mkutano mkubwa wa hadhara.

Tunaomba wapenda haki wote kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi 5/1/2013 katika ofisi za chama Ngarenaro,kwa ajili ya kwenda kutoa misaada hiyo kwenye vituo vya Yatima,pia tunatoa wito kwa kila mmoja wetu kujitolea chochote anachoweza Sukari/mchele/sabuni/mafuta etc kama ishara ya kutoa Sadaka,kwa Mwenyenzi Mungu ili HAKI iweze kutendeka.

Tutaendelea kudai haki na usawa katika jamii yetu hata kwa gharama ya maisha yetu.Denis na Ismail pamoja na wengine wengi tutawakumbuka daima,damu yenu hakimwagika bure,

No comments: