Tuesday, March 19, 2013

RIPOTI MAALUMU KUHUSU KESI YA KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI KENYA

Taarifa kutoka 254 zinasema tayari kesi iliyowasilishwa na mrengo wa CORD imesajiliwa na mahakama ya upeo nchini Kenya na tayari jopo la majaji watano limeteuliwa kusikiliza kesi hiyo akiwemo rais wa Mahakama ya Upeo Dr. Willy Mutunga huku msajili wa Mahakama akithibitisha kwamba watakaosalia kusikiliza kesi hiyo ni majaji sita kinyume na kawaida ambapo huwa ni saba.

Kesi inatarajiwa kuanza kusikilizwa leo march 19 2013 Nairobi kenya na endapo mrengo wa CORD utatoa uthibitisho kwamba uchaguzi ulikua na dosari, duru ya pili ya uchaguzi itaandaliwa chini ya siku 60 ambapo mrengo wa CORD unawakilishwa na mawakili kama Mutula Kilonzo na Moses Wetangula ukidai tume huru ya uchaguzi haikuzingatia mipangilio wa uchaguzi kama vile kutambua wapiga kura kupitia mitambo ya kielektronik.

No comments: