Tuesday, March 19, 2013

LULU MICHAEL ALIKUMBUKA PENZI LA STEVEN KANUMBA.....

Wakati zikiwa zimebaki wiki chache tu hadi kifo cha Stephen Kanumba kitimize mwaka mmoja, aliyekuwa mpenzi wake, Elizabeth Michael aka Lulu kwa mara ya kwanza leo ameandika ujumbe kuhusiana na jinsi anavyomkumbuka.

Lulu aliachiwa kwa dhamana mwezi January mwaka huu baada ya kukaa mahabusu kwa takriban miezi minane kufuatia kukamatwa kwa kuhusika na kifo cha Kanumba.
Lulu ambaye hivi karibuni amekuwa akitweet mara kwa mara ameandika:

“Ulikuwa zaidi ya baba,kaka,mpenzi,mume,ndugu,rafiki….sitoacha kukulilia katika maisha yangu yote!!R.I.P daddy angu STEVEN KANUMBA.”

Akiambatanisha na picha ya Kanumba, Lulu ameongeza, “I will alwayz love u daddy angu!”

No comments: