Wednesday, April 10, 2013

MVUA YALETA MAAFA WILAYANI ARUSHA WANANCHI KADHAA HAWANA MAHALI PA KUISHI

 Hali ya mvua inayonyesha kwenye mkoa wa Arusha imewaacha wakazi wa vijiji vya Alkokola na venginevyo kadhaa kwenye kata hiyo wilaya ya Arusha wakiwa hawana makazi na mahala pakukaa baada ya mvua kunyesha usiku wa kuamkia Jumatatu.
Pichani ni maji yakiwa yanashuka kwenye maeneo ya Ngaramtoni ya Chini na Burka huku wakazi wa maeneo hayo wakiyakimbia maeneo yao kama walivyokutwa na kamera yetu.

No comments: