Tuesday, January 8, 2013

EDWARD LOWASSA AVIPIGA JEKI VIKUNDI SABA VYA VIKOBA MONDULI MJINI

 Mh. Lowassa akikabidhiwa zawadi na mwenyekiti wa Vikoba Kijiji cha Monduli Juu, Dawson Kaaya
wakati viongozi wa vikundi hivyo walipomtembelea nyumbani kwake Monduli.
 Mmoja wa viongozi wa vikundi vya vikoba Kijiji cha Monduli Mjini akisoma risala mbele ya Mh. Lowassa.
 Baadhi ya wanavikoba wa Monduli Mjini wakimsikiliza Mh. Lowassa (hayupo pichani).
Mhe Edward Lowassa akipewa zawadi na Bi Arafa Ismail kutoka katika vikundi vya Vikoba Monduli mjini ambao walikwenda kumtembelea nyumbani kwake. Kushoto kwa Mhe ni Bw. Dawson Kaaya ambaye ni Mwenyekiti wa Vikoba Monduli Mjini.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa amevipatia vukundi saba vya Vikoba vilivyopo Wilayani Monduli, kiasi cha shilingi milioni nane kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao. Lowassa amesema yeye ni mkereketwa mkubwa wa Vikoba huku akisisitiza kuwa ni chachu ya maendeleo na kumkwamua Mtanzania kutoka katika umasikini. Kila kikundi kimepata shilingi millioni moja ambapo kikundi kilichofanya vizuri kimeongezewa shilingi milioni moja zaidi.

No comments: