Tuesday, January 8, 2013

SANII WA MNANDA OMAR OMAR AFARIKI DUNIA

MSANII  nyota wa miondoko ya Mnanda 'Mchiriku', Omar Omar, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Habari zilizotufikia ni kwamba, Omar Omar aliyetamba na nyimbo mbalimbali ukiwemo ule maarufu wa 'Kupata ni Majaliwa' alifariki nyumbani kwao Temeke, saa chache baada ya kurejeshwa kutoka Hospitali ya Temeke alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.
Taarifa hizo zinasema kuwa mara baada ya kurejea nyumbani, msanii huyo alizidiwa na hatimaye kufariki na msiba wake upo nyumbani kwao Temeke Mikoroshini.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amen!

No comments: