Tuesday, January 8, 2013

LIONEL MESSI ATWAA TUZO YA BALLON D'OR

                            Lionel Messi akiwa na tuzo yake ya Ballon d'Or.
                       Fabio Cannavaro, akionyesha jina la mshindi wa Ballon d'Or, Lionel Messi.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi, ameshinda tuzo ya Ballon d'Or kwa mwaka wa nne mfululizo.
Messi (25) alifunga jumla ya mabao 91 mwaka jana na aliwashinda wachezaji wengine Andres Iniesta wa Barcelona na Christiano Ronaldo wa Real Madrid.

Messi alitangazwa mshindi wa tuzo hiyo ya the Ballon d'Or, tuzo ambayo hukabidhiwa mchezaji bora wa mwaka katika sherehe iliyofanyika mjini Zurich.
Mesi sasa ni mchezaji wa kwanza kuwahi kushinda tuzo hiyo ya Ballons d'Or kwa miaka minne mfululizo na kuvunja rekodi ya aliyekuwa mchezaji wa Ufaransa na rais wa UEFA kwa sasa, Michel Platini, ambaye alitwaa tuzo hiyo mara tatu mfululizo mwaka 1983, 1984 na 1985.

Hapa chini ni orodha ya kikosi cha wachezaji bora wa mwaka 2012
•Iker Casillas (Real Madrid)
•Dani Alves (Barcelona)
•Gerard Pique (Barcelona)
•Sergio Ramos (Real Madrid)
•Marcelo Vieira (Real Madrid)
•Andres Iniesta (Barcelona)
•Xabi Alonso (Real Madrid)
•Xavi Hernández (Barcelona)
•Cristiano Ronaldo (Real Madrid)
•Radamel Falcao (Atletico Madrid)
•Lionel Messi (Barcelona)


No comments: