Thursday, March 7, 2013

MAAFANDE WAHUSISHWA NA TUKIO LA UTEKAJI WA MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI, ABSALOM KIBANDA HII NI KAULI YA ABSALOM KIBANDA BAADA YA KUTEKWA...............

"Baada ya kutoka kwenye gari, nahisi nilikanyaga sehemu mbaya, nikateleza na

kuanguka wakanifuata...niliona kama watu watatu hivi wakaanza kunishambulia.

Sikuwa nafahamu kilichojiri, lakini nilisikia mwingine akimwambia mwenzake

afande 'mshuti... mshuti' huyo alipoelekeza mtutu na kujaribu 'kushuti'

(kupiga risasi) ilikuwa kama vile imegoma.

“Nikiwa bado niko chini, wakanipiga kwa kitu cha ncha kali kwenye jicho la

kushoto, wakaning’oa meno na kucha katika vidole vya mkono wa kulia,

walinipiga sana na nilipata maumivu makali. Baada ya kunipiga na kunijeruhi

waliniburuza hadi bembeni ya nyumba yangu na kunitupa na wakaondoka, baadaye

majirani na wasamaria wema walikuja kuniokoa..."

No comments: