Saturday, June 23, 2012

UJERUMANI YATINGA NUSU FAINALI EURO 2012

Beki wa Ujerumani, Philipp Lahm akishangilia pamoja na Jerome Boateng, bao la kwanza aliloifungia timu yake dhidi ya Ugiriki leo wakati wa mechi ya robo fainali ya michuano ya Euro 2012 katika uwanja wa Manispaa jijini Gdansk, Poland. Ujerumani wameshinda 4-2. (Picha zote na Alex Grimm/Getty Images)
Bastian Schweinsteiger wa Ujerumani (kulia) akichuana na mshambuliaji wa Ugiriki, Giorgos Samaras wakati wa mechi ya robo fainali ya michuano ya Euro 2012 katika uwanja wa PGE jijini Gdansk, Poland. Ujerumani wameshinda 4-2. (Picha na REUTERS)

TIMU ya taifa ya Ujerumani imefanikiwa kutinga nusu fainali ya michuano ya Euro 2012 baada ya ushindi wa 4-2 dhidi ya Ugiriki kwenye mchezo wa robo fainali ya michuano ya Euro 2012 katika uwanja wa  PGE jijini Gdansk, Poland. Mabao  ya Ujerumani yamefungwa na Philipp Lahm, Sami Khedira, Miroslav Klose, na Marco Reus.

No comments: