Friday, January 4, 2013

RAIS KIKWETE AONGOZA MAMIA KUMZIKA JUMA KILOWOKO 'SAJUKI' JIJINI DAR LEO

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la marehemu Sadick Juma Kilowoko 'Sajuki' leo.
                  Baba mzazi wa Sajuki, Mzee Kilowoko, akiweka udongo katika kaburi la mwanaye
                                                                   Mazishi ya Sajuki yakiendelea.


                                                   Umati wa watu waliohudhuria mazishi hayo.

MAMIA ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam leo wamejitokeza katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam kumpumzisha mpendwa wao Sadick Juma Kilowoko 'Sajuki' aliyefariki dunia alfajiri ya Januari 2, mwaka huu (Jumatano) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Miongoni mwa waliomzika Sajuki ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete

No comments: