Tuesday, July 31, 2012

Halmashauri Arusha angalieni usalama wa watu hawa!

 Baadhi ya wafanyabiashara wakiwa wamepanga bidhaa zao kando ya barabara na kuacha nafasi kidogo isiyoruusu magari kupishana, pia kujaza takataka nyingi katika mtar wa maji taka unaopita kando ya barabara hiyo.

Baadhi ya madereva wa Jijini Arusha wamelalamikia kitendo cha Halmashauri ya Jiji la Arusha kuruhusu shughuli za ufanyaji biashara kando kando ya barabara nje ya Soko Kuu la Arusha kwa kuwa mara kwa mara kumekua kukitokea kwa ajali na kusababisha hasa ya mali na maisha ya watu.

Madereva hao wasema kuwa wafanyabiashara hao wamekuwa wakigongwa na wengine kufa huku pia wateja nao wakigongwa na magari au pikipiki.

No comments: