Tuesday, July 31, 2012

BALOZI WA PAPA NCHINI TANZANIA ATOA SAKRAMENT YA KIPAIMARA KWA MARA YA KWANZA KATIKA KANISA LA MT. PETRO OYSTERBAY

 Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini, Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, akimpaka mafuta ya kipaimala Theodory Helon,  wakati wa ibada ya Sakaramenti ya kipaimara iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Osyterbay jijini Dar es Salaam jana. Jumla ya watoto 72 walipata sakramenti hiyo, kushoto ni mzazi wa kiroho  wa mtoto huyo, Daniel Mwisongo.
 Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini,  Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, akimkabidhi Aivan Catrece, zawadi ya msalaba  wakati wa ibada ya Kipaimara iliyofanyika katika kanisa la mtakatifu Petro Osyterbay jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya watoto kati ya 72 waliopata sakaramenti ya kipaimara wakionyesha vyeti vyao baada ya kukabidhiwa na Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini Askofu Mkuu Fransisko  Padilla, wakati wa ibada hiyo iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Osytarabay jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, akikabidhiwa zawadi ya mbuzi na Catrece Theodory ambaye ni mmoja wa wajumbe wa kamati wakati wa Ibada ya kipaimara iliyofanyika jana katika kanisa la mtakatifu Petro oysterbay jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Paroko wa parokia hiyo Joseph Mosha.
 Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, akiwahutubia watoto wa kipaimala  wakati wa ibada ya sakaramenti iliyofanyika katika kanisa la mtakatifu Petro Osyterbay jijini Dar es Salaam, Jumla ya watoto 72 walipata ekaristi hiyo.
 Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, akitoa baraka kwa waumini wa kanisa la Mtakatifu petro Oysterbay wakati wa Ibada ya Kipaimara,Askofu huyo ilikuwa mara yake ya kwanza kuongoza ibada katika kanisa hilo ambapo alisalimiana na waumini wote kwa kuwapa mikono na baraka.
Balozi wa baba Mtakatifu hapa nchini Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, akitoa baraka kwa waumini wa kanisa la Mtakatifu petro Oysterbay wakati wa Ibada ya Kipaimara,Askofu huyo ilikuwa mara yake ya kwanza kuongoza ibada katika kanisa hilo ambapo alisalimiana na waumini wote kwa kuwapa mikono na baraka.
Mmoja wa watoto waliopta sakaramenti ya kipaimara katika kanisa la Mtakatifu Petro, Aivan Catrece, akionyesha kipaji chake cha kupiga ngoma wakati wa Ibada hiyo.

No comments: