Tuesday, July 31, 2012

TAARIFA ZA MIKOA TOFAUTI KUHUSU MGOMO WA WALIMU PAMOJA NA KAULI YA WAZIRI.

Chama cha walimu Tanzania kimeanza mgomo wa walimu nchi nzima july 30 2012 ambao unatokana na walimu laki moja na elfu 53 kuukubali.

Ishu imekua nzito baada ya kushindwa kupata kile walichotaka kwa serikali ndani ya siku 30.

Wanachotaka ni kulipwa malimbikizo, ongezeko la mishahara kwa asilimia 100, posho za kufundishia kwa walimu wa sayansi asilimia 55 na walimu wa sanaa asilimia 50 na posho za mazingira magumu kwa asilimia 30.

Shinyanga walimu waliendelea na kufundisha kama kawaida, ambapo walimu wengi wakuu wamesema hawana taarifa zozote za kuanza kwa mgomo, yani hawakuambiwa chochote na bado wanaendelea na kazi.

Dar es salaam shule nyingi kumekua na mgomo mfano Mbezi Luis ambako wanafunzi walikwenda hadi kituo cha polisi Mbezi Luis kwa maandamano.

Kwenye mkoa wa Tanga shule kadhaa zimeonekana kuwa kimya huku wanafunzi wakiwa wenyewe shuleni, walimu wamegoma na wanafunzi kubaki kucheza tu na wengine wakarudi nyumbani.

Kwenye mkoa wa Pwani mgomo ulikuepo ambapo kwenye shule ya Mkoani wanafunzi walikua nje baada ya walimu kuondoka ambapo mwandishi wa habari Victor kasema kwenye shule ya Mtongani Mlandizi wilayani Kibaha ilikua kimya na imefahamika walimu waliwachapa wanafunzi walioingia darasani.

Amesema kwenye shule ya msingi Maili Moja mgomo ulikuepo ambapo baadhi ya wanafunzi walikua wakipiga mawe kwenye ofisi za walimu ambazo milango yake ilikua imefungwa, walimu hawajafanya chochote toka asubuhi.

Singida na Mbeya pia kumekuwepo na mgomo, kwa upande wa Mbeya kwa mujibu wa mbeyayetu Blog kuna vurugu kubwa ambayo mpaka Polisi waliingilia na kupiga mabomu ya machozi kutawanya wanafunzi walioandamana kushinikiza walimu wawape mitihani kabla ya kufunga shule.

Pamoja na hizo taarifa zote za mgomo, Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Dr Shukuru Kawambwa amesema mgomo huo ni batili lakini Serikali inawahakikishia walimu ambao hawajajihusisha na mgomo kwamba Serikali na vyombo vya usalama vitawalinda na kuwahakikishia usalama wao.

Amesema “tunawatahadharisha Walimu wote ambao wamegoma na wamekua wakiwatishia maisha walimu wengine ambao hawako kwenye mgomo, atakaebainika hatua za kisheria zitachukuliwa”

No comments: