Saturday, July 7, 2012

Ziara ya Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Washington DC

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi naUsalama Mhe. Edward Lowassa alimkabidhi Bw. Hayes zawadi kutoka Tanzania ikiwa ni ukumbusho wa ziara yao kwenye taasisi hiyo.
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. KhalifaKhalifa (MB) akifuatilia maelezo ya Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Africa Mashariki ya USAID Bibi Susan Fine, walipokuwa kwenye mkutano na maafisa wa ofisi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara ya wabunge hao mjini Washington DC, Marekani. Picha inayofuata ni ujumbe mzima wa kamati hiyo pamoja na maafisa ubalozi wa Tanzania Washington DC.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe.Edward Lowassa(Mb.) akimkabidhi Bibi Susan Fine zawadi za vinyago vya kuwekea mishumaa baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. RachaelMasishanga Robert (Mb.) akimvalisha afisa wa USAID ushanga uliotengenezwa na wajasiriamali wa Tanzania baada ya kumaliza mkutano.

                                                      Picha ya pamoja.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nje, Ulinzi na Usalama wakiwa na KaimuBalozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Lilly Munanka kwenye mkutano na Corporate Council on Africa, taasisi ya Marekani inayotoa ushauri wa kibiashara na uwekezaji barani Afrika

Kamati ilikutana Rais wa Taasisi hiyo Bw. Steven Hayes ambaye alielezeafursa nyingi wanazotoa kwa balozi mbalimbali za Afrika hapa Washington DC ili kuvutia wafanyabiashara na wawekezaji wa Kimarekani kwenda nchi hizo za Afrika

Katika mkutano huo Bw. Hayes alisifu jitihada za ubalozi wa Tanzania na Balozi Mwanaidi Maajar kutumia kituo hicho mara kwa mara kwa nia ya kutafuta maeneo ya ushirikiano na kuwahamasisha wawekezaji wa Kimarekani kuwekeza Tanzania.

No comments: