Monday, July 16, 2012

JACQUELINE ABADILI DINI

MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini Jacqueline Massawe ambaye ni maarufu kwa jina la WOLPER amesisitiza kwamba amebadili dini na kwa sasa anajiandaa kwa kuupokea na kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumza katika chombo kimoja cha habari Luninga WOLPER amesisitiza kwamba yeye hivi sasa ni muislamu na amejitayarisha kufunga na kujizuia kufanya shughuli za kisanii ambazo zitamsababishia kutengua saum yake hivyo kwa kipindi hicho cha muda wa mwezi mmoja atakuwa akijishughulisha na kazi zake zingine.

"Unajua dini ni imani na hii iko ndani ya moyo wangu hivyo nachukizwa kwa kitendo cha baadhi ya ndugu zangu wa karibu kuniita MALAYA na hukumu kwa mambo mbalimbali mimi ndiyo najua na fanya nini katika maisha yangu"alisema.

Aidha amewatupia dongo wale wote wanao mmtupia maneno ya kumdhihaki kwamba hatoweza kufunga na kuswali , "Unajua tumepewa miezi 11 ambayo tuko huru kufanya mambo mbalimbali ya starehe za kidunia kwanini nishindwe kujizuia ndani ya mwezi mmoja tu, mimi nasema hivi  nitasali sitakuwa na makucha , manywele  na mambo mbalimbali ambayo hayapendezi katika ibada "

No comments: