Monday, July 16, 2012

SMZ YANDAA MIKAKATI YA KUPAMBANA NA UINGIZAJI WA DAWA ZA KULEVYA ZANZIBAR

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeandaa mikakati ya kudhibiti dawa za kulevya ili kuweza kupambana na uingizwaji na utumiaji wa dawa hizo nchini .

Akijibu suala la Mhe Ismail Jussa ladhu jimbo la mji mkongwe alietaka kujua hatua gani zinachukuliwa na Serikali kuweza kudhibiti madawa ya kulevya nchini, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais ,Fatma  Abdulhabib Fereji  alisema wizara yake itahakikisha mikakati hiyo inafanyakazi ili kuona Zanzibar inakuwa salama na utumiaji wa dawa za kulevya.

Amesema janga la dawa za kulevya halina mipaka na kuathiri mustakbali wa rasilimali na nguvu kazi ya taifa, hivyo juhudi zinahitaji kuchukuliwa katika kuzuiya matumizi ili kuwaepusha vijana kutumbukia katika janga hilo.

Mh. Fatma amesema katika kipindi cha mwaka 2010 kuanzia novembar hadi disemba ni kesi 67 zilizokamatwa na januari 2011 hadi juni 2011 ni kesi 168 na kuanzia julai 2011 hadi juni 2012 ni kesi  104.
Alieleza kuwa katika harakati hizi za kupambana na udhibiti wa dawa  za kulevya na uhalifu kwa ujumla  umepungua kutokana na kuimarisha ulinzi shirikishi na taasisi za  dola  kufanya doria mitaani pamoja na kuandaliwa kikosi maalum kikosi kazi ambacho hufichua maficho ya watumiaji na wauzaji dawa za kulevya .

No comments: